Zaburi 124

Kama Bwana asingalikuwa upande wetu; Israeli na aseme sasa: kama Bwana asingalikuwa upande wetu, wakati watu walipotushambulia, wakati hasira yao ilipowaka dhidi yetu, wangalitumeza tungali hai, mafuriko yangalitugharikisha, maji mengi yangalitufunika, maji yaendayo kasi yangalituchukua. Bwana asifiwe, yeye ambaye hakuruhusu turaruliwe kwa meno yao. Tumeponyoka kama ndege kutoka mtego wa mwindaji; mtego umevunjika, nasi tukaokoka. Msaada wetu ni katika jina la Bwana, Muumba wa mbingu na dunia.

Neno: Biblia Takatifu

copyright © 1984, 1989, 2009, 2015 Biblica, Inc — CC-BY-SA-4.0 — CC-BY-SA-4.0

订阅我们的新闻通讯

及时了解新的资料页、活动与平台更新。